Tuesday, March 3, 2020

TENDO LA NDOA




SEHEMU YA KWANZA
Maisha ni zawadi tunayo pewa wote na mwenyezi Mungu! maana hakuna ata mmoja anaelipa pesa mara tu pale anapo kuwa amezaliwa. Lakini hayahaya maisha yanaweza kukufanya wewe ujutie kwa nini uliletwa hapa duniani.
Sasa mnamo mwaka 1995, kijana Alexander alionekana kuwa kijana mchapakazi, mwelevu, alikuwa mwenye heshima, na alipendwa na kila mtu kule kwao.
Lakini siku moja jamani, alexander aliumia sana nakujutia kwanini alizaliwa duniani. Maana ilikuwa ni siku ya jumamosi siku ambayo alexander na mama yake mzazi pamoja na bibi kizaa mama yake walikuwa wote nje ya nyumba  pembezoni kabisa ya mlango wakiwa wote wanakula mahindi ya kuchemshwa na wakiwa wanafurahia kwa pamoja.
Mama yake alexander akasema,
"Jamani mimi ngoja niwaache maana tayari nimechelewa kwenye shughuli zangu"
Wakamjibu "sawa we wai maana leo umechelewa"
Mama alexander akasema,
"Haya sawa, lakini alexander mwanangu mkimaliza kula mahindi kusanya vigunzi pamoja kisha ukavitupe visizagae ovyovyo hapa nje."
Alexander akajibu "sawa mama nitafanya hivyo"
Baada ya mama yake kuondoka alexander akajisahau baada ya kula muhindi wake kigunzi akaanza kukichezea kwa kukirusha juu na kukidaka.
Sasa alipo kosea kudaka kumbe kigunzi kikawa kimedondoka na kuangukia upande wa pili pale pale nyumbani kwao.
Sasa wakati alexander ameenda kuchukua maji ya kunywa ndani, bibi yake masikini akawa amebanwa na haja ndogo, ndipo akaamka polepole maana alikuwa ni mzee tayari, sasa wakati anatembea kuelekea chooni, masikini mguu wa kushoto wa yule bibi ukawa umekanyaga kile kigunzi ndipo bibi akawa ameteleza vibaya na kupasuka kichwa na kufariki hapohapo. Sasa alexander wakati anachukua maji akasikia kishindo kikubwa nje! alipo toka nje akakuta jamani bibi yake ameanguka na anatokwa damu masikioni, puani, mdomoni na akawa amepasuka vibaya sana kisogoni! Alexander alipo enda kumtazama alishangaa sana kuona tukio kama lile, alipo jaribu kumuita kwamba "bibi amka bado nakupenda bibi" hakuamka masikini.
Alex alipo angalia kile kigunzi kilicho mdondosha bibi dohh ni yeye alikitupa pale
na mama yake aliacha amemuelekeza asitupe vigunzi ovyo. Ndipo alex akaamua..
USIKOSE SEHEMU YA PILI                       




















SEHEMU YA PILI
No_2
Alexander masikini alipo gundua bibi yake kuwa amefariki! ndipo akaamua kukimbia na kutoroka nyumbani kwao bila ata kumuaga mama yake mzazi. Na wakati mama yake alex alikuwa anampenda sana mwanae na alikuwa anamtegemea sana maana ndiye alie kuwa mtoto wake wa pekee.
Alex aliogopa sana maana alijua ni yeye amemuua bibi yake.
Sasa wakati alexander yupo njiani akiwa anatoroka kuelekea sehemu asiyo ijua! Alex masikini alisahau ata kumfunika marehemu bibi yake pale nje ya nyumba akamuacha bibi akiwa na damu na akiwa ameachama mdomo wake na kukodoa sana macho pale alipo fariki.
Kipindi alex yupo njiani anatoroka baadhi ya watu walikuwa wanamuonea huruma! Maana alex alikuwa analia na kutokwa machozi kipindi yupo safarini masikini dahh.
Mama yake alex alikuwa bado hajatoka kazini, na alikuwa hana taarifa yoyote kama mama yake mzazi amefariki kule nyumbani,
Sasa ilipo fika mida ya jioni kipindi alex bado yupo njiani akiwa analia sana mpaka macho yake kubadilika rangi na kuwa mekundu, mvua masikini alianza kunyesha sana, na kilicho kuwa kinauma zaidi ni pale mvua ya barafu ilipo kuwa inanyesha na kumnyeshea marehemu bibi pale nje!
Masikini wa mungu mwili wa marehemu bibi ulinyeshewa sana pale nje bila mtu yeyote kugundua na alisikitisha sana watu! pale siafu zilipo kuwa zikiutembelea mwili wa marehemu bibi pale nje.
Sasa siku ya kwanza ikapita bila mtu yeyote kujua kama bibi amefariki, maana ata mama yake alex alipata dharula kazini kwake hivyo akawa amelala kazini na ukizingatia hata simu hazikuwepo sana kipindi kile, labda angepiga simu kwa alex ili aweze kumjulisha.
Ila sasa mama alex alipo rudi nyumbani  alipitia mlango wa nyuma pale nyumbani,
alishangaa sana kuona ukimya mwingi wakati alizoea kukuta alex akicheka na kutaniana sana na bibi yake. Alijaribu kuwaita lakini hakuna alie itika ata mmoja.
Mama  Alipatwa na wasiwasi sana ndipo akaamua kutoka ndani kwenda kuchungulia sehemu walipo kuwa wanakula mahindi.
Alishituka sana kukuta mama yake ameanguka chini na akiwa ana majelaha makubwa sana isitoshe tena alikuwa amefariki. Alipo angalia akakiona kigunzi kilivyo mwangusha yule bibi mpaka kumtoa kucha za miguuni.USIKOSE YA_3                       
SEHEMU YA 3
Mama alex alisikitika sana, aliumia nakusema kwamba "mwanangu alex kwanini umefanya hivi, kwanini umemuua mama yangu jamani?, nitawambia nini ndugu zangu mimi jamani, nitaificha wapi sura yangu! baba yetu aliisha fariki na tulimbakiza mama tu sasa na yeye amefariki sababu yako alex mwanangu, nilikuzuia kutupa vigunzi ovyo hapa nyumbani"
Mama Alex aliongea haya maneno huku akiwa analia! mpaka misuri ya kichwa akaanza kuvimba! Alilia na mvua ikimnyeshea! mpaka mapovu yakaanza kumtoka mdomoni!
Mungu saidia baada ya mvua kupungua ndipo majirani wakaanza kuzisikia nduru na kilio kutoka kwa mama alex!
Dooh walipo fika walisikitika sana  kumkuta yule bibi amefariki maana alikuwa anapendwa sana na majirani zake.
Ila mama Alexa alishangaza sana watu masikini! yani Kipindi watu wote wanajadili jinsi gani wataushughulikia mwili wa marehemu.
Walishanga jamani, kumuona mama alex amevua nguo zake zote na kubaki uchi wa mnyama bila kuogopa ata watoto! Akisema kwamba, "nakuraani mwanangu alex kwa kumuua bibi yako, popote ulipo usifanikiwe ata kwenye ndoa yako"
Dooh wakina mama walivua vitenge vyao  na kumfunika mama alex ili asibaki uchi uku wakimfariji na kumtia nguvu.
Sasa wakati alex yupo njiani akiwa anaondoka sehemu asiyo ifahamu, alisafiri sana yani mpaka pesa yake  ikawa imekaribia kuisha.
alex alikuwa anawaza sana maisha yake yatakuwaje kule aendapo, ndipo yule dada alie kuwa amekaa na Alex siti moja kwenye basi akamuuliza "kaka samahani mbona kama unamawazo sana"
Alex akajibu, " hapana dada yangu ni mambo ya dunia tu wala sina tatizo"
Yule binti akamuuliza " mimi naitwa Fadhira, wewe unaitwa nani?
Ndipo akamwambia "mimi naitwa Alex"
Ila wakati Alex na Fadhira wanazungumza walitokea kupendana sana! lakini hakuna ata mmoja alie mwambia mwenzake!
 Sasa Walipo fika mkoa wa Shinyanga! Ilikuwa imeisha fika usiku, ndipo waliamua kutafuta sehemu ya kulala wageni, yani "GUEST HOUSE"
lakini bahati mbaya walipata chumba kimoja tu!
Dah ikabidi wakubaliane kulala wote hicho chumba!
lakini bahati mbaya masikini Fadhira alikuwa na majini mabaya sana na yalikuwa hayamruhusu yeye kulala na mwanaume yeyote yule..
USIKOSE YA 4
Mtunzi @hadithizetu #0769510060                       




















SEHEMU No_4
Alex na Fadhira walipo kubaliana kulala  chumba kimoja, alex hakuwa na wasiwasi wowote lakini Fadhira masikini alikuwa muoga kiasi na wasiwasi pia maana alikuwa analijua tatizo lake mwenyewe, kwamba akilala tu na mwanaume yeyote yule mashetani yake lazima yaamke.
Alitamani kumwambia Alex kwamba wasilale wote, lakini Fadhira alikuwa muoga akahisi kwamba akimwambia alex wasilale wote, alex atamuhisi yeye ni mchoyo.
Hivyo basi akaamua kukaa kimya moyoni mwake, mapigo yake ya moyo yalikuwa yanaenda kasi, maana alijua lazima cha moto atakipata chumbani.
Walipo pewa ufunguo wa chumba chao, Fadhira aliupokea ufunguo, na walipo fungua chumba na kuingia ndani Fadhira alifunga chumba kwa ndani nakuuficha ufunguo chini ya kapeti! Ili mashetani ya kimpanda, Alex asije kumkimbia, maana yale mashetani yalikuwa yanamtesa sana.
Baada ya kila mmoja kuoga walilala, na wote walikuwa wamechoka sana, hakuna ata mmoja alietaka kumsumbua mwenzake siku iyo.
Lakini Alex anasema kwamba, hatasahau ilipo fika saa sita na dakika sita na sekunde sita yaani 666. Upepo mkali ulitanda mule chumbani! Alex alishangaa na alishtuka sana akaangalia saa yake ni saa sita.
Dooh upepo ulizidi chumbani masikini, na kibaya zaidi Fadhira alikuwa hasikii chochote kile.
Alex akamuamsha akisema kwamba "rafiki yangu amka, kuna upepo mkali Fadhila"
lakini alishangaa kuona  haamki! Na mwili wa fadhira ulikuwa mzito maana alikuwa hajigeuzi, yaani kama mtu aliye kufa.
Dooh Alex aliogopa akihisi labda mzimu wa marehemu bibi yake imemfata.
Alianza kulia  kwa uoga akisema "nisamee bibi yangu nihurumie naogopa bibi"
Kumbe haukuwa mzimu wa bibi yake bali yalikuwa ni yale majini na mashetani ya fadhira! Na mashetani siku zote yalikuwa yanakuja kwa njia ya upepo.
Kipindi alex anawaza akisema "nyumbani nimeacha bibi yangu amekufa, sasa jamani na hapa tena huyu dada amekufa, dooh mikosi gani huu"
alishangaa kusikia Fadhira anaamka na kupiga kelele, na sauti kubadilika ikawa ya kiume ikisema "kwanini mke wangu unalala na wanaume wakati nimeisha kutolea maali na mizimu inakutambua" Alex aliogopa masikini, maana Fadhira alianza kujipiga kichwa chake chini mpaka damu nyingi kumtoka.
Usikose ya 5
SEHEMU YA: NO_5
Kipindi mizimu inaendelea kumtesa  Fadhira masikini, alikuwa anapiga kelele sana, akisema "nakufa mimi, naumia jamani msinisukume"
Alex alikuwa anashangaa maana alikuwa hamuoni anae msukuma!
Alex akaongea kwa uoga kwamba "Fadhira jamani ndiyo umeamua kuniogopesha hivi, siungesema kama hutaki tulale wote"
Alex masikini alizania labda ni masiara.
Lakini alikuwa anashangaa Fadhira anajipiga kichwa chake chini tena sana na damu zikimtoka pia.
Alex alijaribu kutafuta funguo ili atoroke lakini hakuzipata maana Fadhira alikuwa amezificha
Hivyo kutokana na kelele Fadhira alizo kuwa anapiga masikini, wateja wote kwenye ile "GUEST" wakaamka na kuanza kushangaa! ndipo mlinzi wa guest akaja kugonga mlango ili Alex afungue lakini Alex hakuwa na ufunguo,
mlinzi akasema, "Jamani mbona mnasumbua wateja wetu kwa kelele zenu hizo"
Alex yeye hakuweza kujibu maana alikuwa anaogopa sana masikini na alikuwa anamkimbia fadhira mule ndani kwa kujibana kwenye kona za chumbani
Fadhira alikuwa anamuinulia mkono Alex ili Alex amshike kichwa chake, asiendelee kukipiga chini, Lakini alex alikuwa anaogopa anahisi labda majini yata mdhuru na yeye
Basi masikini kwa sababu fadhira alikosa msaada na alikuwa kajipasua sana kichwa chake, dooh Fadhira alikufa mbele ya macho ya Alex jamani!
Alex alilia kama mtoto akisema kwamba. Jamani "kwanini nimelala na mtu nisiye mjua"
Dooh mlinzi na wateja wa guest walipo ona alex hafungui ndipo wakaanza kubomoa mlango ili waangalie kinacho endelea ni nini?
Walikuta yule binti amekufa wakasema "wewe kijana ndiyo umemuua huyu dada" Alex alilia akisema "sio mimi ni mizimu"
Wakamjibu "usizani sisi ni wapumbavu amekunyima mapenzi umemuua"
ALEX ANASEMA KWAMBA,
walimpiga sana masikini, mpaka mikono na miguu yake ikalegea. Sasa walipo mlegeza mikono na miguu. Ndipo wakamwambia achimbe kabuli mwenyewe kisha amzike Fadhira peke yake, Alex alichimba kaburi mwenyewe. Ikafika hatua akachoka ata shimo halikuwa refu! ndipo akamzika  dada wa watu hivyohivyo! maana ata ndugu zake Fadhira walikataa kumfata ndugu yao sababu ya majini yake! Fadhira alizikwa bila ata jeneza jamani alifunikwa shuka tu la mule Guest.
USIKOSE YA 6
MwandIshi FRANK DAVID @hadithizetu





















SEHEMU NO_6
Alex alipomaliza tu kuzika,akamfata muhudumu wa ile gest akamwambia nashukuru sana,umenisaidia nimenusurika na polisi asante ila nataka kuendelea na safari yangu.
muhudumu akamwambia "nani kakwambia nimekunusuru na polisi, mauji yako pale pale na wewe ni muuaji hapa hauruhusiwi kuondoka mpaka boss aje na nimeshampigia simu aje na polisi"
Alex akatoa macho tu.
akamwambia "kaka naomba unisamehe tafadhari, yani hapa nilipo sina hata mwenyeji katika huu mji tafadhari sijamuua mimi ni mizimu yake imemuua"
yule mhudumu akamwangalia Alex juu mpaka chini alafu akamuuliza "utanipa shingapi nimpigie boss asije" Alex akachoka kabisa akijiangalia mfukoni ana elfu 8 tu, akamwambia mhudumu aliyejulikana kwa jina la kisukuma Maganga,
 "Maganga hapa mfukoni nina elfu 8 tu! sidhani kama elfu 8 inaweza kununua kesi nzito kama hii? sina pesa na wala sina neno tena la kuongea"
Maganga akamwambia "shida yangu ni laki 1 tu sawa? nipatie hiyo pesa nikuruhusu"
Alex akasema "sina" kwa unyonge akawa anaiona jela inamkaribia masikini.
Maganga akamwangalia Alex kwa jicho la dharau afu akamwambia
"hapa gest niko peke yangu kuna kijana uha anakuja na kunisafishia hapa na ninamlipa kila siku elfu 1, siku nyingine anapenda niziweke ziwe nyingi nimpe, sasa unatakiwa kuanzia leo uwe unasafisha hii gest na kufua mashuka yote  mpaka laki 1 ninayoitaka itimie yaani hapa unakaa miezi3 na siku10"
Alex kusikia vile alifurahi sana jamani,  huku akimshukuru maganga na kusema bora mateso ya uraini kuliko jela, basi kuanzia siku hiyo alex akawa anafanya usafi hapo gest akimaliza anatoka kwenda kuzurula na kula mitaani jioni anarudi gest kuvizia sehemu ya kulala kama mwezi mmoja, mpaka akawa ameishazoeleka na boss akamjua! alikuwa mkarimu mpole ila alikuwa na sifa ya kusahau na kupuuzia jambo.
Siku moja usiku sana giza tele, mzimu wa Fadhira ulimtokea Alex, na kibaya zaidi mzimu wa fadhira ulikuja ukiwa uchi! yani mtupu kabisa jamani dah na mzimu ulikuwa umechafuka sehemu zake za siri,  matiti yakiwa waziwazi mzimu ukasema, "alex rafiki yangu naomba unifufue jamani! sijafurahi umenizika na pedi naitaji kuzikwa nikiwa msafi,naitaji kusafishwa"
USIKOSE 7,                           
@hadithizetu
Sehemu 7
Alex aliogopa sana masikini pale mzimu wa Fadhira ulipo mtokea usiku wa manane.
Alex akauliza ule mzimu kwa uoga sana kwamba "Fadhira kwa nini umekuja ukiwa uchi?" Mzimu wa Fadhira ukajibu huku ukiwa unalia eti kwamba "Alex rafiki yangu nimekuja nikiwa uchi sababu nilikuwa nakupenda sana Alex, na wala usiniogope siwezi kukudhuru ila nimeumia sana yani umenizika mimi nikiwa nimevaa pedi chafu naitaji kuwa msafi kama wafu wengine jamani nakosa furaha kabisa nikiwa na wafu wengine! nifufue Alex, maana usipo nifufua mimi na kunivua ile pedi, sitochoka kukufata popote uendapo"
Palepale baada ya mzimu wa Fadhira kutamka yale maneno ukapotea ghafla.
Alex alishituka sana! Ndipo akaamka mida ya saa tisa usiku akachukua koleo pamoja na jembe alilo mzikia Fadhira kisha akaenda kumfufua kwenye kaburi lake.
Alex masikini alienda akiwa analia akisema "bibi yangu asinge teleza na kigunzi nisinge pata haya mateso yote"
Alex alipo fika makabulini alitazama mbele na nyuma hakuna mtu, kushoto na kulia pia hakuna mtu, ndipo Kijana Alex akaanza kuchimba kaburi ili amfufue Fadhira kisha amtoe ile pedi na amzike upya. Kweli alianza kuchimba kwa roho moja tu ila Alipo fika katikati ya kaburi dooh harufu mbaya sana ya kuoza ikaanza kunuka! Maana mwili wa marehemu Fadhira ulikuwa umekaa mda mrefu pia
Alex alijaribu sana kujikaza na ile harufu ili angalau aweze kumfufua Fadhira lakini kadri alivyo kuwa anachimba harufu ilianza kumzidi na kumfanya ajihisi kuumwa.
Alex alivua t_shirt lake kisha akajifunika puani mwake ili harufu ipungue ili aendelee kuchimba lile kaburi lakini harufu masikini ilimfanya alex azidiwe.
Wakati alex amechimba akauona mkono wa marehemu, kipindi anaushika mkono kuuvuta juu akatoka na nyama za mkono zilizo kuwa zimeoza zimekuwa laini.
Kijana Alex Anasimulia na kusema kwamba. Alikaa kwanza chini akalia jamani, alilia akisema kweli maisha ni zawadi kutoka mbinguni lakini maisha pia ni adhabu. Alex alichimba shimo kweli kisha akamtoa binti Fadhira mpaka juu, dah Fadhira alikuwa amejaa wadudu aina ya Funza kwenye mwili wake yani atamaniki kabisa, na wakati ameisha mvua nguo zake sasa ili kumtoa ile pedi.....
USIKOSE_8


SEHEMU : NO_8
Alex alipo mvua nguo zote marehemu Fadhira, kipindi sasa anataka kuitoa ile Pedi, dah masikini! akawa amekamatwa na mlinzi wa yale makaburi, Mlinzi akamwambia "wewe mchawi unafanya nini usiku huu makaburini, kwa nini unafufua miili ya wafu gizani?"
Alex aliogopa sana! ndipo mlinzi akaanza kupiga kelele, wana kijiji wote wakaja pale wakiwa na panga pamoja na marungu na kuanza kumpiga sana Alex!
Dooh yule boss mwenye guest akasema, "msimuuwe huyu ni kijana wangu tumuulize kwa nini anafanya hivi ili tujue tunamsaidiaje"
Wanakijiji  wakasema,
"hatumtaki hapa Alex ni mchawi na amzike marehemu aliye mfufua kisha aondoke kutoka hapa aende kwao"
Dah masikini Alex aliinama na kuanza kumzika upya binti Fadhira huku akiwa anachapwa viboko na mwenyekiti wa mtaa, bila ata kufanikisha kuitoa ile pedi.
Alex alifukuzwa kama mnyama masikini na kuacha sifa mbaya ya uchawi.
Kipindi alex yupo kwenye basi linaloenda jijini Dar, mzimu wa fadhira ulimtokea kwenye basi umo umo dooh Alex alianza kutetemeka sana.
Mzimu ukasema "Alex kwa nini umenizika mchafu, kwa nini bado hujanitoa pedi "
Alex akajibu, "nilijaribu nikashindwa nimepigwa sana kwa ajili yako"
Mzimu wa fadhira ukasema "Alex najua unatambua nimekufa, lakini nimekufa nyama sijafa roho, nateseka sana huku nilipo, natengwa na kila kiumbe sababu ya hiyo pedi naonekana mchafu jamani! Na mimi nimeisha kufa hivyo siwezi kutoa mwenyewe naomba nitoe pedi wewe Alex shuka kwenye basi rudi shinyanga kaburini kwangu kanitoe ile pedi tafadhari"
Dooh watu kwenye basi walimshangaa sana kijana Alex wakawa wanamuangalia yeye tu yani basi zima! wakijadiriana kwamba "huyu kaka ni kichaa au? mbona analia na kuongea mwenyewe"
Maana walikuwa hawauoni mzimu wa Fadhira wala sauti ya mzimu.
Alex peke yake ndiye alie kuwa akiuona ule mzimu.
Kwenye lile basi kulikuwa na wachungaji wa kilokole .na mapadri wote imani zao hazikuwaonyesha ule mzimu.
Hata hivyo mule kwenye basi pia  kulikuwemo na IMAMU kiongozi wa msikiti
Imamu aliamka kutoka kwenye siti yake akamfata Alex kisha akamwambia kijana unateswa sana na mizimu, Imamu akatoa TASUBII kisha akaanza kuufukuza ule mzimu..
USIKOSE YA 9
.





















SEHEMU No_9
Baada ya IMAMU kuomba. Alimsaidia sana Alex, maana  mzimu uliacha  kumtokea safarini.
Walipo fika jijini Dar, Alex alikuwa hajui wapi pa kuelekea! maana hakuwa na ndugu wala mtu yeyote yule alie kuwa anamfahamu.
Sasa wakati Alex yupo mjini aki shangaa shangaa!
Alibanwa na haja ndogo masikini! Ndipo akaenda kukojoa pembeni kwenye ukuta wa kanisa!
Sasa wakati anakojoa,mchungaji wa kanisa akamuona! Kisha akamuita, "kijana njoo hapa" Alex hakuwa muoga akaitika  kisha akaenda,
Mchungaji akasema "kwanini unakojoa kwenye eneo la kanisa, tena kwenye ukuta wa mungu" Alex alishangaa kisha  akasema "nisamee, nilikuwa sijui kama ni vibaya, maana kule kijijini kwetu tunakojoa sehemu yoyote tu mkojo unapo kuwa umekubana " mchungaji alikasilika kisha akasema "naona unanijibu kwa dharau sio, ngoja nikupe adhabu"
Alex alipewa kazi ya kufyeka eneo la kanisa, dooh kusema kweli Alex alipewa eneo kubwa jamani afyeke"
kijana Alex kwakuwa alikuwa mpole na ndiyo ilikuwa mala yake ya kwanza kuja Dar na hakuwa na pakufikia hivyo akafanya adhabu yake tena kwa roho moja!
Alifyeka eneo la kanisa vizuri sana kwa mda mchache tu.
Mchungaji alivyo toka nje kukagua eneo alishangaa sana akasema "kijana nani amekusaidia kufyeka, maana umefanya kazi nzuri! ndani ya mda mchache! vijana wengi uwa nawalipa pesa zangu lakini wanafanya kazi ovyo ovyo"
Alex akajibu "mchungaji mimi napenda sana kazi"
mchungaji akamuuliza, "wewe unaitwa nani na unaishi wapi?"
Alex akasema jina lake kisha akasema "mchungaji mimi sina sehemu yoyote ya kuishi nimekuja dar leo alafu sina ndugu wala mzazi uku mjini,nipo nipo tu"
Mchungaji alipenda sana uchapakazi na ukalimu wa Alex, akamwambia "kijana sio vizuri kuzurula humu mjini utateseka sana kijana wangu, ila nimependa uchapakazi wako naomba ubaki hapa kwangu uwe unanisaidia kazi za hapa na pale kisha nitakuwa nakulipa kwa mwezi.
Alex alifurahi sana masikini kisha akafanya kazi kwa roho moja.
Sasa baada ya miaka kadhaa kupita, Alex alikuwa tayari ameokoka na alikuwa ameisha jenga nyumba yake nzuri ya kuishi!
Ndipo akaamua kumuoa binti wa yule mchungaji,
Na hapa ndipo laana za mama yake na bibi yake Alex, zikaanza kumtokea!
Usikose 10
Mtunzi @hadithizetu
0769510060                   




















 No_10.
Alex alimuoa Rose yule mtoto wa mchungaji, lakini Rose alikuwa ana virusi vya ukimwi masikini, na Alex alikuwa hajui!
Sasa siku moja usiku Alex na Rose, wakiwa wamelala kitandani, wote walipata hisia ya kufanya tendo la ndoa.
kipindi Alex anampapasa Rose, Alex Alishangaa sana kumuona marehemu Fadhira anamtokea! akisema,
"Alex usifanye hilo tendo nakuomba tafadhari"
Alex akajibu nisifanye kwa nini na huyu ni mke wangu?"
Mke wa Alex akasema "mme wangu jaman yani unanivua nguo alafu unaongea mwenyewe mbona sikuelewi"
Rose alikuwa hausikii mzimu ukiongea,

Dah Alex akaishiwa hamu siku hiyo na hakufanya chochote kile!
ila Mke wa Alex alichukia sana hiyo siku  maana alikuwa na hamu.
Walikaa miaka mitano bila kufanya tendo la ndoa kwa usumbufu wa mzimu! Na Kila walipo jaribu kufanya ilishindikana, ila walikuwa wakijilizisha kwa njia zingine tu.
Baada ya miaka kadhaa kupita mama Alex, umri wake ulikuwa umaenda sana na alitamani sana mwanae Alex aje nyumbani kumjulia hali maana hakuwa na mtoto yeyote yule zaidi ya Alex!
Ikabidi mama aende kwa mganga wa jadi ili amuangalizie Alex alipo, maana miaka ilikuwa mingi ajarudi kwao.
Mganga akamwambia mama Alex "ukitaka ujue mwanao alipo njoo leo usiku saa tisa ukiwa uchi"
Mama Alex alifanya hivyo sababu ya mapenzi ya mwanae!
Mama Alex alipelekwa ziwani akiwa uchi! Akapakwa dawa, kisha mganga akamwambia "nyanyua matiti yako , kisha sema Alex mwanangu njoo unyonye,Popote alipo atasikia tu"
Baada ya kumaliza vile wakaondoka.
Kesho yake Alex, kichwa kilimuuma sana jamani, ndipo akaamua kurudi nyumbani mapema! Alipo fika kwake akaingia mpaka ndani, Hakuamini macho yake, alifumania mkewe anafanya ngono zembe na kiongozi wa kwaya ya kanisa.
Alex alisema "mke wangu unafanya nini hichi"mke akasema "sijafanya kitu"
Alex akasema, angalia shuka langu mmelichafua, jitazame ulivyo sweti, angalia hujavaa nguo ya ndani upo uchi! unasema hujafanya kitu, Rose akasema mme wangu mimi nimechoka kuvumilia miaka mingi sasa bila kufanya "TENDO LA NDOA" nimezidiwa mme wangu....
NINI HATIMA YA KIJANA ALEX USIKOSE YA 11 @hadithizetu                       


















TENDO LA NDOA SEHEMU YA 11.
Kijana alex aliumia sana masikini , maana alikuwa anampenda sana mke wake akamuuliza swali tena maana hakuamini kabisa kama amesalitiwa.
“mke wangu kwanini umeamua  kufanya hichi kitu yani unanisaliti tena ndani ya chumba changu kwenye shuka langu mwenyewe”
Mke wa alex akasema “ mme wangu naomba unisamee najua nimefanya kosa kutoka nje ya ndoa lakini halikuwa kusudio langu ni shetani tu kanipitia na kibaya zaidi ni kwamba mme wangu tumeishi wote miaka mingi mpaka sasa lakini haujawai kufanya chochote na mimi nimeshawishika nilipo pata hamu mpaka uvumilivu umenishida”
Alex akamwambia Yule kiongozi wa kwanya ya kanisa kwamba ,
“kaka hivi kumbe wewe ni mkristu hewa? Na kwa nini usiache kufundisha ata hii kwaya  yetu, maana una dhambi nyingi sana kaka,
 Alex akasema mimi sina chochote kile cha kukufanya wewe ila naomba utoke ndani kwangu ukiwa uchi uende mpaka kwa mke wako alipo”
Yule mchungaji wa kwaya bwana  petron akaanza kulia akisema
“alex mwana mkristu mwenzangu, naomba unisamee, naomba unihurumie maana naogopa kwenda nje nikiwa uchi kumbuka mke wangu ame hokoka na anaheshimika sana sasa nikitembea uchi  uko  nje uoni kama nitakuwa namuahaibisha,jamii itanitazamaje mimi jamani, nihurumie  Alex”
Alex alikuwa amekasilika sana jamani akasema “tangu  nimezaliwa sijawai kusamehewa na hapa nilipo nimepitia matatizo mengi sana! Hivyo ata wewe siwezi kukusamehe.
Kweli alimnyanganya Yule mwalimu wa kwaya ya kanisa ile suti yake kisha akamtoa nje kama mwizi akamwambia ondoka na akafunga mlango .
Yule mwalimu wa kwaya masikini akafumba macho yake kwa haibu kali sana mtaani akaenda kwa kujificha akiwa uchi masikini mpaka kwake kila mtu alikuwa anamtazama watoto walianza kumcheka na watu wote wakashangaa sana masikini.
Mwalimu wa kanisa alipo fika kwake mke wake akamuuliza” mme wangu unatoka wapi na kwanini upo uchi”
Mme wake akasema” nisamee mke wangu sitarudia ni shetani tu”
Mke wake akajibu “nikusamee nini”
Mme wake akasema “nimetembea na mke wa  alex Yule mwenyekiti wa kanisa na huyohuyo alex ndiyo amenifumania na kunifukuza kwake nikiwa uchi, nashindwa kukuficha maana watu wote nje wameniona  nikiwa uchi na wanajua kosa nililo tenda ila nisamee sana mke wangu ni kosa tu limetokea bahati mbaya”
Mke wa mwalimu wa kwaya ,alikuwa ni yatima na alikuwa anamtegemea mme wake kwa kila kitu hivyo akaamua kumsamee maana hakuwa na sehemu yeyote ile ya kuegemea zaidi ya kwa mme wake.
Lakini dah kumbe masikini Yule mwalimu wa kwaya alikuwa ameambukizwa ukimwi na mke wa alex hivyo  akauleta ugonjwa pia mpaka ndani kwa mkewe masikini dooh.
Alex hakuwa na jinsi pia ila akamwambia mke wake kwamba “kwani umeshindwa kuchukua mwanaume yeyote Yule mpaka umeamua kuchukua mme wa mtu tena mkristu mwenzetu laana gani unaleta ndani ya familia”
Mke wake akasema nisamee sitarudia tena mme wangu.
Baada ya ya wiki mbili kupita, alex na mke wake wakiwa chumbani usiku wamelala huku wakiwa wanachezacheza kitandani  mzimu wa fadhira ulikuja umejaa vidonda mwili mzima!
akasema “alex kwanini unataka kufanya mapenzi na huyo mwanamke wakati ameathirika”
 alex akasema  “mke wangu ni mtoto wa mchungaji  hawezi kuathirika na ukimwi” mzimu ukamuuliza kwamba “kwani umempima mke wako kufahamu afya yake au unamuamini tu kwa macho”
Mke wa alex akashituka kisha akasema “alex mme wangu kwanini unaota ndoto za ajabu namna hii, yani unaniota kuwa mimi nina ukimwi huoni kama unanikosea sana mme wangu”
Alex akasema sio ndoto ni fadhira amekuja masikini
Mzimu wa fadhila ukasema ”Alex naomba usimwambie mke wako kuhusu mimi tafadhali”
Alex akanyamaza kimya!
Mke wa alex akaanza kulia sana akasema naona sahivi huniamini yani nakusikia kwa masikio yangu ukisema kwamba mimi nina ukimwi.
Alex akamuuliza fadhira “ kwanini sasa hivi umechafuka sana umejaa vidonda mwili mzima, kwanini usivae nguo unakuja uchi kila siku”
Fadhira akasema ulikataa kunisafisha nateseka sana huku nilipo, natengwa, nanuka ,nachekwa sababu ya uchafu lakini sina jinsi nimeisha zoea kwa sasa”
Baada ya mzimu kuongea yale maneno ulipotea ghafla!
Palepale mke wa alex akaanza kugomba sana akisema kwamba “yani wewe unasema mimi nina virusi vya ukimwi kumbe unaishi na mimi alafu uniamini sio naomba kesho mapema twende hospital tukapime na kama sina utanikoma mimi ni nani”
Alex hakuwa na jinsi aliamua kukubali tu sasa walipo fika hospital masikini kweli mke wa alex alikuwa ameathirika ila alex alikuwa hajapata bado maambukizi ya virusi vya ukimwi! dooh  Alex alimuogopa sana mke wake akasema  “mimi siwezi kuishi na wewe tena, sitaki kuugua ukimwi, alafu kumbe fadhira alikuwa ananiambia ukweli”
Doctor akasema hapana alex kijana wangu usifanye hivyo, huyu ni mke wako wa ndoa kama ulivyo sema  hapo awali kipindi unataka kupima, sasa ukimkimbia utakuwa hujafanya vizuri maana ata kama anaukimwi unaweza kuishi nae na ukatumia njia mbadara na usiweze kupata maambukizi.
Alex alisema sawa doctor ngoja nikaongee na wazazi wake ili niweze kulimaliza ili swala.
Kweli masikini alex aliwaita wazazi wa mke wake, kisha akawambia mimi na mototo wenu tumepima leo ila mke wangu amekutwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi! hivyo siwezi kuishi nae tena, na mahari niliyo toa nimeisamee, nyumba yangu namuachia yeye aishi mimi nataka kurudi kwa mama yangu  mzazi.
Wazazi wa mke wa alex hawakuwa na jinsi ikabidi wakubaliane na mawazo ya alex, ila alex akaulizwa swali, kwanini hukumpima kipindi unataka kumuoa, alex akasema mimi nilizania kuwa kwakuwa mkemwangu ni mtoto wa mchungaji hivyo hawezi kuwa na mgonjwa  ya zinaa kama haya.
Mke wa alex aliwekwa kwenye maombi na kanisa lao zima ili aweze kuponywa  maana tayar alex alikuwa kaisha mkimbia, sasa mwalimu wa kwaya alipo sikia zile habari za kwamba mke wa alex ana ukimwi moja kwa moja akajua na yeye lazima ukimwi anao maana hakutumia kinga alipo fanya nae,
dooh mwalimu wa kwaya alipo enda kupima yeye na mkewe wakakutwa wote wawili wameathirika masikini, dah mke wa mwalimu wa kwaya alikua anauogopa ukimwi hivyo akawa amejiua maana alikuwa anaogopa aibu za watu kwamba amekonda sana sababu ya virusi.
Mke wa alex alilia pia na akakimbia kutoka mkoa ule na kwenda sehemu asiyo ifahamu maana alikuwa anakwepa haibu za watu.
Sasa alex akaamua kuanza safari kurudi nyumbani kwa mama yake maana hakuwa na sehemu yoyote ya kukimbilia, sababu akuwa na ndugu yeyote isitoshe kule shinyanga na penyewe aliacha jina baya sana masikini.
Sasa kipindi alex yupo njiani akakutana na bibi mmoja amezeeka sana masikini alafu Yule bibi alikuwa mchafu sana, yani alikuwa anatoa mpaka harufu chafu,
kibaya zaidi alikuwa amebeba mzigo mkubwa sana kichwani, alex alishikwa na huruma jamani akamkumbuka bibi yake kipindi yupo mzima alikuwa anamsaidia sana kazi ngumu ngumu na wala alex alikuwa hapendi kumuona bibi yake anafanya kazi nzito ya kumchosha kama yule bibi alivyo kuwa amebeba,
alex akamfata kisha akamwambia “bibi naomba nikusaidie mzigo” bibi alinyamaza kimya na alex alikuwa bado hajamuona usoni, dooh alex akarudia tena “bibi umebeba mzigo mzito sana naomba nikusaidie maana unateseka sana”
Yule bibi akamjibu kwamba “asante kijana wangu lakini kama kweli una huruma kwa wazee kwanini hukumsaidia bibi yako nyumbani kwenu alipo kufa, alafu unataka kunisadia mimi” alex alishituka sana masikini dah akasema kwani bibi yangu umemjuaje?
USIKOSE SEHEMU YA 12                       

















SEHEMU YA 12
Kijana alex alisikitika sana kwa maneno ambayo Yule bibi aliyaongea, aliamua kunyamaza kimya kisha akasema,
“bibi naomba kama unafahamu chochote kuhusu bibi yangu uniambie”
Yule bibi akasema “kama kweli unataka ufanikiwe na maisha yako  rudi nyumbani ukamzike bibi yako, rudi nyumbani ukamuone mama yako mzazi”
Alex akasema “sawa nimeelewa bibi yangu, lakini bado sijajua wewe ni nani”
Yule bibi hakujibu chochote, na hapo hapo akapotea kama upepo!
Alex alishtuka sana masikini, akaogopa pia maana alijiuliza maswali mengi kwanini iwe hivyo kwanini huyo bibi amtokee kwa njia kama ile?
Na Kule nyumbani kwa kina alex, mama yake alex aliugua sana masikini na hakukua na mtu yoyote Yule wa kumuuguza, dooh mama alex alikuwa analia akisema,
“hivi mwanangu amekuwaje jamani kwanini ameniacha nateseka sina mtoto mwingine zaidi yake bora angekuwepo hapa nisinge teseka maana pesa sio kila kitu”
Na mda huohuo alex alikuwa yupo njiani anaelekea kwao!
Mama ake alex akarudi kwa mganga wake kisha akamuuliza mbona mtoto wangu haji? na kama matambiko tumeisha fanya, mimi nakosa furaha pale ninapo jiuguza mwenyewe wakati nimeisha wai kuzaa, mama alex akaendelea kusema kwamba mganga ni bora tufanye matambiko upya labda mwanangu anaweza kurudi.
Mganga akamjibu mama alex kwamba, mtoto wako lazima arudi wewe usiwe na haraka,
mama alex alirudi kwake akiwa analia huku akisema huyu mganga ni muongo ananipa tu moyo.
Sasa kipindi alex anarudi kwao mzimu wa fadhira ukamtokea tena masikini ukamwambia alex naomba nisaidie kitu,
Alex naomba urudi mkoani shinyanga ukachukue mchanga juu ya kabuli langu kisha ukae nao popote uendapo ili nisiweze kukutokea tena maana nahisi nakuchosha ninapo kutokea nataka kukuacha huru na mimi nipumzike pia, fadhira akasema sitakutokea tena lakini usirudiane na mke wako.
Alex hakuwa na jinsi alifanya kama alivyo ambiwa, sasa kipindi alex anarudi kwao akamkuta mama yake ayupo, alex alikuwa bado anakumbuka sehemu wanapo kuwa wana ifadhi ufunguo! ndipo akaufata ufunguo ili aweze kufungua mlango wao aingie ndani.
Kweli alikaa ndani ili amsubilie mama yake,
 kipindi alex amekaa ndani alishangaa kuona picha ya bibi yake ukutani
Alex alifata ile picha akaikumbatia akasema bibi yangu popote ulipo naomba unisamee, hazikupita ata dakika tano, alex alisikia sauti isemayo
“nimekusameee, Nimekusamee mjukuu wangu,na mimi ndiye Yule bibi nilie kutokea nikakwambia uje kwenu! Nimekusamee kwa roho moja maana hukuniua wewe ila ilikuwa mipango ya mungu, na ninajua fika kuwa ulikimbia kwa kuogopa kwamba raia kwenye asila kali wange kuuwa wakizani uliniua, msubili mama yako pia umuombe msamaa maana aliku laani akiwa uchi wa mnyama.
Alex aliendelea kulia akijutia maisha yalivyo mpiga hakutamani kabisa kuishi tena lakini alikuwa anajikaza, sasa wakati kijana alex yupo nyumbani anamsubilia mama yake mzazi aje ali amuombe msamaa, alishangaa sana kuona watu wanakuja nyumbani tena baada ya masaa mawili wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa mama yake dooh!
Alex alilia kama mtoto masikini, alijigalagaza.
Akauliza nani amemuua mama yangu?
Wakamjibu alex kuwa kuna dada amemgonga mama yako barabarani na gari, lakini aliye mgonga alitaka kukimbia tumemkamata na tumempiga mpaka amefariki,
Alex akalia zaid mpaka akatokwa na jasho lisilo pimika
Akasema “nionyesheni huyo mtu natamani sana nimuone.”
Kweli walimchukua alex wakampeleka mpaka eneo la tukio kisha wakamuonyesha alie muuwa,
Dooooh masikini alex alilia zaidi maana kumbe alie mgonga mama yake na gari mpa kumuuwa alikuwa ni Yule mke wake mtoto wa mchungaji, hivyo vilio vikawa mala mbili.
Maisha ya alex yalikuwa machungu kwa takribani kama miaka sita, na siku moja usiku alex alimeza sumu akitaka kujiua lakini majrani walimsaidia kwa kumpa maziwa ili asife, kipindi alex anapiga kelele akitaka kukata roho.
Alex aliendelea kuishi kama kichaa, na watu walishangaa sana kuona anaongea ongea mwenyewe kila mda akisema,
“SINA BABA, SINA MAMA ,SINA BIBI, SINA MKE”
Alex alikuwa akiongea hayo maneno kila mda. kila saa, bila ata kupumzika
Ndugu na jamaa walimuonea sana huruma, na mala nyingi walikuwa wakimletea chakula pamoja na kumfanyia usafi wa mwili wake maana alex alikuwa anajisahau ata kuoga kwa msongo  wa mawazo
Ndipo Kijiji kilikaa chini nakusema kwamba,
MAMA ALEX ALIKUWA MAMA MMOJA MZURI SANA, NA ALIPENDWA NA KILA MTU,  WAKUBWA NA WADOGO PIA,
 HIVYO LEO HII AMEFARIKI HATUWEZI KUITAZAMA FAMILIA YAKE INAANGAIKA SANA HIVI, NI  BORA TUMTAFUTIE HUYU KIJANA ALEX MKE,
 ILI AISHI NAE NDANI LABDA ANAWEZA KUKAA VIZURI SIKU MOJA.
Wanakijiji wote walikubaliana na yale mawazo na hakuna ata mmoja alie pinga lile swala
Kweli wanakijiji walijichangia pesa kwa ajili ya mahari ya binti atakae olewa, maana kimila walikuwa wanatoa ngombe.
Pesa zikapatikana lakini hakuna ata binti mmoja alie kubali  kuolewa na kijana alex.
Mabinti wote walisema kwamba “kijana ni mchafu na anaongea mwenyewe kama kichaa nani aishi nae, dooh tena kwanza ali laaniwa na mama yake na ndiyo maana yupo vile, hatumtaki sisi hatuwezi kuishi na bwana kama yule”
Wanankijiji walichoka kumtafutia alex mke, hivyo wakashindwa ni jinsi gani wanaweza kumsaidia aweze kuishi vizur,i ikabidi wamuache alex kama alivyo.
Alex aliendelea kukaa ndani kwa tabu bila kuoga wala kula vizuri alex alianza kutoa harufu kitendo kilicho mfanya mpaka yeye mwenyewe kutoka ndani nakuanza kutembea nje kama vichaa wengine,
Kumbe masikini wa mungu ni zile laana za mama yake zilikuwa zinafanya kazi.
Alex aliteseka sana jamani, maana aliacha nyumba yake bila mtu yoyote kukaamo mpaka nyumba ikaanza kuota magugu na kuchakaa kama pango.
Siku moja usiku alex akiwa amelala mzimu wa mama yake mzazi ukamtokea na kusema kwamba
“NIMEKUSAMEE MWANANGU, HAMKA, RUDI NYUMBANI”
Palepale jamani ukichaa ukaisha alex akaanza kujishangaa ilikuwaje mpaka akawa chizi, alex alikuwa hatambui, alex alijishangaa yupo kwenye mauchafu jalalani, ndipo akaamua kurudi mpaka kwao akiwa na aibu tele
Alex alishangaa kukuta vinyesi nimepakwa ukutani kwenye sebure yao ,kumbe ni yeye  alifanya vile kipindi anaumwa uchizi.
Wanakijij walishangaa sana kumuona alex amepona. Watu wakamwambia alex jinsi mabinti walivyo mkataa alivyo taka kuozeshwa.
Alex alipo ingia chumbani kwa mama yake alikuta nyoka mkubwa sana chumbani na kibaya zaidi Yule nyoka hakuwa na nia ya kumdhuru, bari nyoka aliingia uvunguni na kisha akapotelea humohumo. Wakati alex ameinama uvunguni akitaka kumuuwa Yule nyoka papo hapo alishangaa kukuta begi lenye milioni 200 za mama yake mzazi alizo kuwa ameziacha.
Kumbe Yule Yule nyoka alikuwa mzimu masikini,
Alex alianza kufanya biashara mpaka akawa tajiri mkubwa wilayani kwao na hakuna mtu yoyote alie weza kumshinda,
 alex alifungua shelli za mafuta alifungua maduka na shule na vitega uchumi vingi, vilivyo mfanya yeye  kuwa na pesa nyingi sana
Wale wadada walio mkataa alex asiwaoe walianza kujileta tena wakiomba msamaa lakini alex aliwakataa wote akasema mke mwema uletwa na mungu maana niliteseka sana nilivyo owa kwa haraka na hata sikufaidi tendo la ndoa……….
MWISHO MWISHO MWISHO WA HADITHI YETU YA TENDO LA NDOA
MTUNZI FRANK DAVID
FACEBOOK INSTAGRAM AND GOOGLE @HADITHIZETU
WHATSAPP +255769510060
CALL ME      +255673510161


Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only